TANGAZO TIGO

TANGAZO TIGO

Wednesday, September 21, 2016

SERENGETI BOYS IMEWATENDEA HAKI WATANZANIA – NNAUYE

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye amesema Serengeti Boys imewatendea haki watanzania kwa kushinda mechi yao ya nyumbani dhidi ya Congo Brazzaville.
“Vijana wamewatendea haki watanzania, tulijaa uwanjani kuwashangilia wamefanya kazi nzuri sana. Timu waliyopambana nayo ni timu nzuri lakini kwa matokeo waliyoyapata ni kutokana na kazi nzuri, mimi nawashukuru nawaombea heri kwenye mchezo unaofuata tunaamini watafanya vizuri”, alisema Mh. Nnauye mara baada ya mechi kumalizika na Serengeti kuibuka na ushindi wa magoli 3-2.
Serengeti inatarajia kucheza mechi yake ya marudiano dhidi ya Brazzaville baada ya wiki mbili huku ikiwa na matumaini ya kukata tiketi ya kusonga mbele kwenye mashindano hayo baada ya kushinda mchezo wa kawanza.CHANZO SHAFFII DAUDA

No comments:

Post a Comment