TANGAZO TIGO

TANGAZO TIGO

Wednesday, November 23, 2016

KIVUMBI CHA KOMBE LA TFF KUENDELEA WIKI IJAYO


BAADA Baruti ya Mara kuifunga Ambassador ya Simiyu mabao 3-1 katika mchezo wa Raundi ya pili  ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC), Uwanja wa Halmashauri ya Kahama, michuano hiyo itaendelea Novemba 27, mwaka huu kwenye viwanja mbalimbali kwa mujibu wa ratiba.

Hatua ya pili itakutanisha timu zlizopenya hatua ya kwanza iliyofanyika wikiendi iliyopita. Mechi zinazotarajiwa kucheza hatua inayofuata ni Tomato dhidi ya Jangwani katika mchezo utakaofanyika mkoani Njombe.

Mbuga FC ya Mtwara itacheza na Muheza United huko Uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara huku Kabela City ya Kahama itakuwa mwenyeji wa Firestone ya Kiteto mkoani Manyara.


Raundi ya tatu itafanyika Desemba 3, 2016 kwa kukutanisha timu za Mtwivila ambayo itasubiri mshindi kati ya Tomato na Jangwani wakati Stand Bagamoyo itasubiri mshindi kati ya Mbuga na Muheza United ya Tanga huku Stand Misuna inasubiri mshindi wa mchezo kati ya Kabela City na Firestone ya Manyara ilihali Mrusagamba ya Kagera sasa inasubiri kucheza na Baruti ya Mara.

Kufika hapo Tomato iliing’oa Mkali ya Ruvuma kwa ushindi wa penalti 6-5; Jangwani iliifumua Nyundo 2-0; Mtwivila iliilaza Sido kwa mabao 7-4; Mbuga iliifunga Makumbusho mabao 5-4; wakati Muheza ilishinda 2-1 dhidi ya Sifa Politan ya Temeke.

Timu ya Stendi FC ililala kwa Kabela City kwa mabao 5-3; wakati Stand Misuna iliifunga Veyula mabao 2-1 huku Stand ikiilaza Zimamoto mabao 5-4 ilihali Baruti FC ya Mara na Mrusagamba ya Kagera zilipita baada ya wapinzani Gold Sports ya Mwanza na Geita Town kugomea mechi za awali kwa kutojitokeza uwanjani.

POSTED BY MINDI JOSEPH

MALINZI AWAPA POLE YANGA KWA MSIBA WA PILI NDANI YA WIKI MOJA


RAIS wa  Shirikisho la Soka Tanzania  (TFF), Jamal Malinzi amewapa pole mabingwa wa nchi, Yanga SC kufuatia msiba wa pili ndani ya wiki moja, baada ya kifo cha aliyewahi kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu, miaka ya 1990, Hamad Kiluvia.

Hamad Kilivua amefariki dunia leo alfajiri Novemba 23, 2016 jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku ambayo Makamu Mwenyekiti wa zamani wa klabu hiyo, Isaac Shekiondo ‘Clinton’ amezikwa kwao Korogwe mkoani Tanga.

Malinzi amesema kifo cha Kiluvia kinaongeza majonzi kwa wana Yanga, kwani kinakuja wakati bado machozi ya kumlilia Shekiondo aliyefariki dunia Novemba 20, mwaka huu kwenye Hospitali ya Amana, Ilala  jijini Dar es Salaam hayajaisha.


Enzi za uhai wake, Kiluvia pia aliwai kuwa Mjumbe wa Bodi ya Seneti ya klabu hiyo pamoja na Malinzi, aliyekuwa pia Katibu Mkuu wa timu hiyo ya Jangwani.

Kadhalika Rais Malinzi alituma salamu hizo kwa familia ya marehemu Kiluvia ndugu, jamaa na marafiki ambayo kwa muda walikuwa wakimuuguza mpendwa wao na hivyo kutokana na kifo hicho, amewataka kuwa watulivu kipindi hiki kigumu cha maombolezo ya mpendwa wao.
.
Msiba wa Kiluvia uko nyumbani kwake, Mikocheni Regent Estate jirani na Ofisi za Baraza la Mazingira (NEMC) ambako taratibu za mazishi zinafanyika. 

POSTED BY MINDI JOSEPH

ARSENAL YALAZIMISHWA SARE 2-2 NA PSG EMIRATES


Alexis Sanchez akikimbia kushangilia baada ya kiungo wa PSG, Marco Verratti kujifungia kuipatia bao la pili Arsenal dakika ya 60 lililoelekea kuwa la ushindi kabla ya PSG kusawazisha na 

mchezo huo wa Kundi A Ligi ya Mabingwa Playa kumalizika kea are ya 2-2 Uwanja wa Emirates. Bao lingine la Arsenal lilifungwa na Olivier Giroud dakika ya 45, wakati ya PSG yalifungwa na Edinson Cavani dakika ya 18 na Alex Iwobi dakika ya 77 aliyejifunga pia.

 Kwa matokeo hayo, Arsenal na PSG zote zimesonga mbele kutoka kundi hilo  

POSTED BY MINDI JOSEPH

MESSI AIFUNGIA MABAO YOTE BARCELONA YASHINDA 2-0 SCOTLAND


Muargentina Lionel Messi akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Barcelona mabao yote dakika za 24 na 55 kwa penalti katika ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji Celtic.

 Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow, Scotland katika mchezo wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Ulaya. Barca imesonga mbele pamoja na Manchester City 


POSTED BY MINDI JOSEPH

MAN CITY YACHOMOA UJERUMANI, SARE 2-2 LIGI YA MABINGWA

Kiungo wa Hispania  David Silva (kulia) akiushuhudia mpira alioupiga ukielekea nyavuni dakika ya 45 na  kuipatia Manchester City bao la kusawazisha .

katika sare ya 1-1 na wenyeji, Borussia Monchengladbach Uwanja wa  Borussia-Park mjini Monchengladbach katika mchezo wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Ulaya. Bao la wenyeji lilifungwa na Raffael dakika ya 23 .

POSTED BY MINDI JOSEPH

Monday, November 21, 2016

SAMATTA ACHEZA DAKIKA SITA TU GENK YAUA 2-0 UBELGIJI

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ametokea benchi na kuisaidia timu yake, KRC Genk kushinda 2-0 dhidi ya AS Eupen katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji.

Samatta aliingia uwanjani dakika ya 84 kuchukua nafasi ya mshambuliaji Mgiriki, Nikolaos Karelis katika mchezo ambao mabao ya Genk yalifungwa na beki wa Mali, Ibrahim Diallo aliyejifunga dakika ya 20 na Alejandro Pozuelo dakika ya 38.

Huo unakuwa mchezo wa 33 kwa Samatta tangu amejiunga na Genk Januari mwaka huu kutoka TP Mazembe ya DRC, 18 msimu uliopita na 13 msimu huu, akifunga mabao nane, matatu msimu huu na matano msimu uliopita
.

Katika mechi hizo, ni 17 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na tano msimu huu, wakati 15 alitokea benchi nane msimu uliopita na 12 msimu huu – na mechi 10 hakumaliza akitolewa, sita msimu uliopita na nne msimu huu
.
Kikosi cha KRC Genk kilikuwa: Bizot, Nastic, Colley, Brabec, Castagne, Ndidi, Pozuelo, Susic/Heynen dk65, Bailey, Buffalo dk76' Trossard) and Karelis (82 'Samatta).
KAS Eupen: Crombrugge, Diallo, Abdourrahman, Diagne, Lazare/Dufour), Garcia, Bassey, Sylla (80 Taulemesse) Onyekuru, Blondelle (88' Hackenberg) Oncansey

chanzo saleh jembe

SIMBA SC YAKUBALI KUTOA SH MILIONI 240 KUREJESHEWA OKWI

SIMBA SC imekubali kulipa dola za Kimarekani 120,000, zaidi ya Sh. Milioni 240 kwa klabu ya Sonderjiske ya Denmark ili kurejeshewa mshambuliaji wake, Mganda Emmanuel Okwi.
Na baada ya Simba SC kulipa fedha hizo, Okwi atarejea kufanya kazi Msimbazi kwa mkataba wa mwaka mmoja kwa mujibu wa makubaliano hayo.


Simba SC ilimuuza Okwi kwa dola 100,000 mwaka juzi Denmark, lakini kutokana na mchezaji huyo kutopata nafasi ya kucheza Ulaya, inaamua kumrejesha na makubaliano yamefikiwa.



"Dola 120,000 tu wale jamaa wanataka watuachie Okwi. Na Okwi naye atasaini kwa mshahara tu mkataba wa mwaka huu, hatumpi dau la kusaini yeye,"kimesema chanzo kutoka Simba. 

Okwi ni mchezaji aliyeipa faida kubwa Simba ndani na nje ya Uwanja enzi zake anacheza Msimbazi. Mbali na kuwasaidia Wekundu wa Msimbazi kushinda matajii mbalimbali tangu ajiunge nao kwa mara ya kwanza mwaka 2010, Okwi pia ameinufaisha kifedha Simba SC
.
Simba ilimuuza Okwi Etoile du Sahel ya Tunisia Januari mwaka 2013 kwa dau la rekodi kwa klabu za Tanzania, dola 300,000, ingawa baada ya muda akaingia kwenye mgogoro na klabu hiyo ya Tunisia.

Mtafaruku ulianza baada ya Okwi kuchelewa kurejea mjini Sousse mkoani Sahel baada ya ruhusa ya kwenda kuichezea timu yake ya taifa, Uganda.

Okwi naye akadai Etoile walikuwa hawamlipi mishahara na kufungua kesi FIFA (Shirikisho la Soka la Kimataifa), ambayo mwisho wa siku alishinda kwa kuruhusiwa kutafuta timu nyingine ya kuchezea kulinda kipaji chake, wakati wa mgogoro wake na klabu ya Tunisia.
Okwi akajiunga na SC Villa ya kwao, Kampala katikati ya mwaka 2013 na Desemba mwaka huo, akahamia Yanga SC.

Hata hivyo, Okwi akavunja Mkataba na Yanga SC Agosti waka 2014, baada ya timu hiyo ya Jangwani kushindwa kumlipa dola za Kimarekani 60,000 kama ilivyokuwa katika Mkataba baina yao na kurejea klabu yake ya zamani, Simba.

Na mapema Oktoba mwaka 2014, Simba SC nayo ilimuuza Okwi  SonderjyskE FC ya Ligi Kuu ya Denmark ambako alisaini Mkataba wa miaka mitano.
Akiwa katika mwaka wa pili wa Mkataba wake wa miaka mitano, Okwi anatarajiwa kurejea Simba tena

chanzo saleh jembe

KOCHA HEMED MOROCCO WA TAIFA STARS ANUKIA STAND UNITED YA SHINYANGA



Baada ya Mfaransa, Patrick Liewig kuachana na Stand United, sasa imeelezwa mikoba yake itachukuliwa na Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Hemed Morocco ambaye tayari ameshafanya mazungumzo ya awali na uongozi wa klabu hiyo.

Morocco ambaye amewahi kuzinoa Coastal Union na Timu ya Taifa ya Zanzibar, ataungana na Athuman Bilal ‘Bilo’ katika kuiongoza timu hiyo inayoshika nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara.

Kwa mujibu wa katibu wa klabu hiyo, Kennedy Nyangi, ni kwamba, baada ya kuwa na mazungumzo na makocha wengi, lakini wamefikia maamuzi ya kukaa chini na kumalizana na kocha huyo.

“Tulikuwa na mazungumzo na makocha wengi ili kuziba nafasi ya Liewig, kati ya hao tumeona Hemed Morocco anafaa kuwa kocha wetu mkuu, kilichobaki kwa sasa ni kuona ni kwa namna gani tunamalizana naye,” alisema Nyangi


chanzo saleh jembe

Sunday, November 20, 2016

MAHAFALI YA 11 YA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA YAFANA JUMAMOSI YA TAREHE 19-11-2016

Sunday, November 20, 2016





Sherehe ya mahafali ya 11 ya chuo cha uandishi na habari na utangazaji Arusha (AJTC) imefanyika mapema jana katika ukumbi wa PPS ikihudhuriwa na wengi  huku mgeni rasmi akiwa ni mea wa jiji la Arusha na diwani wa kata ya Sokoni one Mh  Calist Lazarro.


Sherehe hizo zilianza na maandamano kuelekea ukumbini hapo ambapo shughuli nzima ilifanyika kwa ustadi mkubwa na washereheshaji wakiwa ni Samson Festo na Amosi Thomas Ishengoma ambao walisherehesha mahafali hayo yaliyosubiriwa kwa hamu na walio wengi.

Mgeni rasmi katika mahafali hayo waliohitimu wahitimu 38,Mh Lazarro licha ya kuwataja waliofanikiwa kupitia chuo hicho pia amewataka wahitimu kupambana na sera zinazoibana tasnia kama sera ya mwandishi anayetambulika lazima awe amesoma degree ili kuifikisha mbali tasnia ya uandishi wa habari na utangazaji.


Kwa upande wake mmoja wa wanafunzi waliohitimu hapo jana Bwana Underson Bugoma amesema anamshukuru mungu kwa kumjalia kuhitimu masomo yake salama na kuhaidi atakuwa mwandishi makini na kusimamia ukweli na si kinyume na hapo...

Aidha mmoja wa wanafunzi anayesalia chuoni hapo Bi Asha Kabuga ameeleza kusikitishwa na kuhitimu kwa wanafunzi hao lakini ameeleza kuwa pamoja na kuwapenda na kuwazoea wao bado watawahitaji ili kufika mbali zaidi katika tasnia.

Chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha ni miongoni wa vyuo ambavyo vinatoa mafunzo bora ya uandishi wa habari na utangazaji nchini  na kinashika nafasi ya pili Tanzania kwa mujibu wa NACTE.



posted by MINDI JOSEPH

Tuesday, September 27, 2016

Je, Madrid kufuta rekodi mbovu Ujerumani mbele ya Dortmund leo?

Real Madrid leo wana kibarua kigumu ugenini nchini Ujerumani kucheza na Borussia Dortmund kwenye mchezo wa raundi ya pili ya Kundi F wa UEFA Champions League utakaochezwa kwenye Uwanja wa Signal Iduna Park.
Wakati Real Madrid wametoka kuvutwa na shati kwenye La Liga kwa kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Las Palmas wikiendi iliyopita, Borussia Dortmund kwa upande wao walikuwa na furaha baada ya kuwafunga Freiburg 3-1.
*Borussia wakiwa katika kiwango bora mpaka sasa wameshinda michezo yao yote minne iliyopita katika michuano yote, wakiwa wamefunga magoli 20. Madrid, kwa upande wa wamekosa njaa ya magoli katika safu yao ya ushambuliaji na kushuhudia wakipoteza pointi katika michezo kadhaa iliyopita.
Lakini kocha wa Madrid Zinedine Zidane, ambaye alishinda kila kitu akiwa mchezaji, anaweza kufanya mabadiliko machache kuelekea mchezo huu katika dimba la Sigbal Iduna Park, sehemu ambayo timu imekuwa na historia mbovu kabisa
Kimsingi kwenye mechi zao za mwisho katika uwanja huo kwenye misimu ya 2012, 2013 na 2014, Real hawajashinda mchezo wowote zaidi ya kuambulia vipigo vitatu na sare moja.
Michezo ya hivi karibuni imewapa Madrid matokea ambayo hawakuwa wametarajia. Kiungo mkabaji Casemiro amethibitisha umuhimu wake kwenye timu hiyo na kukosekana kwake katika michezo kadhaa ukiwepo hu wa leo ni pigo kubwa kwa Real kutokana na kukosa muhimili muhimu katika eneo la kiungo mkabaji.
Kutokuwa katika kiwango bora mchezaji Cristiano Ronaldo ni changamoto kubwa kwa ‘BBC’, na hata katika mchezo dhidi ya Las Palmas alitolewa nje kutokana na kushindwa kucheza vyema.
Luka Modric na Toni Kroos watakuwa na kibarua kizito kuhakikisha wanacheza vyema eneo la kiungo, na kuondoa mapungufu yaliyoonekana kwenye baadhi ya michezo iliyopita hasa eneo la kiungo mkabaji ambalo linamkosa Casemiro.
Vilevile, ni vigumu sana kwa James Rodriguez au Isco kupata nafasi ya kuanza kwenye mchezo wa leo kutokana aina ya mchezo wa Dortmund. Dortmund chini ya kocha wao Thomas Tuchel wanacheza soka la kasi ambalo litahitaji umakini mkubwa kwa Madrid katika kuzuia mashambulizi.
Dortmund wanajivunia uwepo wan straika wao aliye kwenye kiwango bora Pierre-Emerick Aubameyang bila kusahau Shinji Kagawa na Mario Gotze ambao lwa pamoja wote watauwasha moto kuhakikisha Dortmund wanapata matokeo.
Wengine ni Ousmane Dembele na Emre Mor ambao pia ni msaada mkubwa kwa wakali hao wa Signal Iduna Park.
Madri wanapaswa kuwa makini zaidi ukizingatia kwamba mpaka sasa Dortmund ndio timu yenye magoli mengi zaidi kwenye Bundesliga, wakiwazidi hata Bayern. Hii inaonesha namna gani walivyokuwa na safu hatari ya ushambuliaji.
Head-to-head statistics 
  • Katika jumla ya michezo yote 10 waliyokutana na Dortmund, Real Madrid wameshinda mara 4, sare mara 3 na wamefungwa mara 3.
  • Katika michezo mitano waliyokutana na Real Madrid Signal Iduna Park, Dortmund hawajafungwa hata mchezo mmoja kati ya mitano, wameshinda mara 3 na kutoka sare mara 2.
  • Mara ya mwisho kukutana ilikuwa ni kwenye robo fainali ya Champions League msimu wa 2013/14. Real walishinda kwa wastani wa mabao 3-2 margin. Mchezo wa kwanza Dortmund walifungwa mabao 3-0 na wao kulipiza nyumbani kwa kushinda mabao 2-0.
  • Real Madrid hawana rekodi nzuri kwa timu za Ujermani wakiwa ugenini kufuatia kufungwa magoli 2-0 na Wolfsburg kwenye robo fainali ya Champions League msimu uliopita. Hata hivyo Real walifuzu baada ya kushinda mabao 3-0 katika mchezo wa marudiano.
CHANZO SHAFFIH DAUDA

Ushindi wa Simba vs Majimaji, Manara atangaza kaulimbiu ya Simba kuelekea October 1







Waswahili husema kipato huleta majivuno, ushindi wa 4-0 ilioupata Simba dhidi ya Majimaji FC, umemfanya msemaji wa klabu hiyo Haji Manara atangaze kauli mbiu ya ‘Wekundu wa Msimbazi’ kwa msimu huu.

 Manara amesema msimu huu Simba haidharau timu timu yeyote kwenye ligi huku akisisitiza timu yake imejipanga kuongoza ligi kudumu hadi mwisho. “Macho yetu na masikio yetu tunaelekeza October 1, ni mechi ya kawaida kama mechi nyingine ya ligi na hatuipi u-special wowote ule. U-special wake ni kwasababu ya kucharuana kwa mashabiki lakini uzito ni ulele tulioutoa kwenye mechi ya Majimaji ndio tutautoa.

 ligi nzima hatutadharau timu yeyote”, amesema Manara mara baada ya mechi kati ya Simba dhidi ya Majimaji. “Tutacheza na Yanga kama tunacheza na mkubwa mwenzetu, hatujali hii ni timu ndogo au kubwa tunatakiwa tuongoze ligi kwa kudumu hadi ligi inamalizika.” “Hatutadharau mechi inayokuja, mechi ya leo ni sawa na mechi inayokuja bila kujali ni Yanga au timu nyingine yeyeyote, kila mechi ni fainali hiyo ndiyo kaulimbiu ya Simba msimu huu.”

CHANZO SHAFFIH DAUDA

Thursday, September 22, 2016

Real Madrid wameshindwa kuvunja rekodi ya Barca La Liga

1Real Madrid wameshindwa kuvunja rekodi ya iliyowekwa na Barca kwenye La Liga ya kushinda mechi 17 mfululizo baada ya kulazimishwa sare na Villarreal katika Uwanja wa Santiago Bernabeu.

Haruna Shamte: Sasa tuko vizuri, naweza kucheza popote katika beki ya City

????????????????????????????????????


MLINZI wa Mbeya City FC, Haruna Shamte ‘Chuma Chakavu’ anaamini kuwa msimu huu wa ligi kuu ya Tanzania Bara ni mgumu ‘kuliko’ lakini kama timu wanataraji kuwa na msimu wa kupenda tofauti na ilivyokuwa msimu uliopita.

Ratiba ya raundi ya nne ya Kombe la EFL hadharani, Mourinho vs Guardiola uso kwa uso tena


1


Droo ya raundi ya nne ya Kombe la Ligi nchini England maarufu kama EFL Cup imefanyika Usiku wa kuamkia leo ambapo timu mbalimbali zimesgajua wapinzani wao.

Barcelona yapata pigo, kumkosa Messi wiki tatu

Staa wa Barcelona Lionel Messi atakuwa nje kwa muda wa wiki tatu baada ya kupata maumivu ya nyonga kwenye mchezo dhidi ya Atletico Madrid uliochezwa Nou Camp na kumalizika kwa sare ya bao 1-1 jana.
Nohodha huyo wa Argentina alipata maumivu hayo punde tu baada ya kumaliza kuwania mpira na beki wa Atletico Madrid Diego Godin na kuanza kuashiria hali ya maumivu hasa kwenye upande wake wa kulia.Jeraha hilo la Messi inaelezwa awali alipata wakati akiwa na timu yake ya taifa ya Argentina wiki chache zilizopita, na staa huyo anatarajiwa kuukosa mchezo wa Champions League dhidi ya Borussia Monchengladbach.
Messi pia atakosa michezo La Liga dhidi ya timu za Sporting Gijon na Celta Vigo, na atakuwa hatihati pia kucheza mchezo wa Champions League dhidi ya Manchester City utakaofanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba.
“Kumkosa Messi maana yake ni pigo katika soka. Tunapokuwa na Messi maana yake tuko imara, lakini tutajitahidi kuwa imara hata bila ya uwepo wake,” kocha wa Barcelona Luis Enrique aliwaambia waandishi baada ya mchezo.

Wednesday, September 21, 2016

SAMATTA NA GENK KATIKA WAKATI MGUMU KIDOGO KAMA MAN UNITED

KRC Genk Jumapili imefungwa mechi ya tatu mfululizo baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Anderlecht Uwanja wa Luminus Arena mjini Genk katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Ubelgiji
.
Mabao yaliyoizamisha Genk katika mchezo huo ambao Nahodha wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta hakucheza kabisa yalifungwa na beki Msenegali Serigne Modou Kara Mbodji dakika ya 64 na mshambuliaji Mtunisia, Hamdi Harbaoui dakika ya 76. 
Genk walipoteza mchezo huo wakitoka kuanza vibaya hatua ya makundi ya Europa League baada ya kufungwa mabao 3-2 na wenyeji Rapid Viena katika mchezo wa Kundi F Alhamisi iliyopita Uwanja wa Allianz, Viena, Austria

.
Na akina Samatta waliingia kwenye mchezo na Rapid Viena wakitoka kufungwa 2-0 na Standard Liege katika Ligi ya Ubelgiji pia. Mara ya mwisho Genk kushinda ilikuwa ni Agosti 28, 2016 waliposhinda 1-0 dhidi ya Zulte-Waregem, bao pekee la kiungo wa Hispania, Alejandro Pozuelo Melero dakika ya 80.
Tangu amejiunga na Genk Januari mwaka huu kutoka TP Mazembe ya DRC, Samatta amecheza jumla ya mechi 25 za mashindano yote, 18 msimu uliopita na saba msimu huu, akifunga mabao nane, matatu msimu huu na matano msimu uliopita

.
Katika mechi hizo, ni 14 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na tatu msimu huu, wakati 11 alitokea benchi nane msimu uliopita na tatu msimu huu – na mechi tisa hakumaliza akitolewa, sita msimu uliopita na tatu msimu huu.

Genk watakuwa na mechi mbili mfululizo ugenini, kuanzia leo Uwanja wa Complex Bredestraat mjini Linter dhidi ya Eendracht Aalst Kombe la Ubelgiji na Jumapili dhidi ya Kortrijk Uwanja wa Guldensporen mjini Kortrijk katika Ligi ya Ubelgiji, kabla ya Alhamisi wiki ijayo kurejea kwenye Europa League watakapoikaribisha Sassuolo ya Italia katika mchezo wa pili wa Kundi F.

Geita Gold Sport yakubali matokeo FDL yalipangwa, soma hapa ilivyokuwa…


JANA nilikuwa nikifuatilia kipindi cha Michezo Times FM ‘Doko-doko’ mwenyekiti wa Geita, Seif Kulunge amekiri kuwa sauti iliyowahi kusambaa katika mitandao ya kijamii ikihusisha baadhi ya viongozi wa Geita Sport na wale wa TFF ni sauti alisi ya kile kilichotakiwa kutendeka.
Amezungumza mengi, ikiwemo la rais wa TFF, Jamal Malinzi kujikopesha zaidi ya Tsh.150 milioni kutoka katika udhamini wa Kilimanjaro.
“Kile kikao (cha upangaji wa matokeo-sauti yake iliwahi kusambaa katika mitandao ya kijamii) kiliitishwa na wahusika wenyewe (baadhi ya watendaji wa TFF) baada ya kuona kwamba plan A imekataa (Geita Sport walikataa kupanga matokeo).
“Kwa hiyo plan B walitakiwa watuite pale ili watueleze kwamba bila milioni 25 ile ‘ngoma itakataa’ na hela zenyewe zilifanyika katika mgawanyo maalumu ulikuwa unaeleweka. Ni nani apewe shilingi ngapi, nani apewe nini.”
“Kwa kweli hicho ni kitu ambacho kinajulikana na watu wenyewe wanafaham kwamba nani na nani walitakiwa wapewe. Kwa hiyo, kwa nafasi fulani sipendi sana kulizungumzia hilo kwa sababu tunataka kuchunguza zaidi pale tutakapopata ripoti ya TAKUKURU.” anasema, Kulunge mwenyekiti wa Geita Gold Sport.
“Moja ya vitu ambavyo vinatakiwa vitolewe taarifa ni hilo. Kwa hiyo kama ni hivyo TAKUKURU wenyewe wanajua, hivyo nikianza kusema mengi hapa nitakuwa navuruga ripoti ya TAKUKURU kiasi ambapo itakapokuja itakinzana.”
“Tuiachie Serikali kwa nafasi yake na muda wake tuone watatuambiaje ili tuamini kwamba hiki kilichokuwa kinasewa ni cha kweli au. Kama kitakuwa ni cha uongo sisi tupo tayari kutoa (ripoti), lakini tutatoa katika nafasi gani, tutajua sisi. Kama ni kwenda ‘kuhiji’ Chato au tunaenda wapi, lakhni tutaitoa.”
“Na leo namwambia Mh. Nape (Waziri wa habari na michezo,) tukishindwa kuyapata hayo kwenye ripoti zake kwa kweli tunaenda kuhiji Chato. Sisi wana Geita tutaenda kuhiji Chato. Wenzetu wanaenda kuhiji Macca, wanaenda Israel, sisi tutaenda kuhiji Chato mpaka kieleweke.” anaongeza kusema, Kulunge.
Kuhusu jina la Jamal Malinzi kuhusika katika kikao cha upangaji matokeo
“Ukweli halisi wa kuhusika kwa jina la Jamal Malinzi katika sauti ile, hatuwezi kufanya kitu bila kuwa na Jamal Malinzi. Timu ile (Geita Gold Sport) baada ya kupata mdhamini, Malinzi alikuwa yuko karibu sana na hiyo timu katika mazingira yote. Na upo uwezekano wa kutumia jina lake ama ikawa ni kweli kwa sababu hata sisi navyokwambia, mpaka yule kocha  wa timu yetu  (Suleimani Matola) aliletwa na Jamal Malinzi.”
“Sisi kocha tuliyemtaka ni Minziro (Fred Felix) ambaye alitakiwa kuja pale, lakini baada ya kuona kwa heshima na taadhima tukamchukua Matola kwa msaada wa Malinzi.” anasema mwenyekiti huyo wa Geita ambayo imeshushwa hadi ligi daraja la Pili.

CHANZO SHAFFIH DAUDA

Kilimanjaro Queens bingwa CECAFA wanawake

Timu ya taifa ya soka la wanawake Tanzania bara, ‘Kilimanjaro Queens’ imefanikiwa kutwaa ubingwa wa baraza vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) baada ya kuifunga Kenya kwa magoli 2-1 katika mchezo wa fainali uliochezwa mjini Jinja nchini Uganda.
Mkongwe Mwanahamisi Omari aliifungia Kilimanjaro Queens bao la kuongoza dakika ya 26 kabla ya Stumai Abdalla kuzama nyavuni dakika ya 44 kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza.
Christine Nafula aliifungia Kenya goli pekee dakika tatu baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kwenye mchezo huo wa fainali.
Safari ya Kilimanjaro Queens ilianza Septemba 9 ikiongozwa na kocha mkuu wa timu hiyo Sebastian Nkoma walikabidhiwa bendera ya taifa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera tayari kuelekea Jinja nchini Uganda baada ya kuhitimisha kambi ya siku chache mjini Bukoba.
Kabla ya kuelekea Jinja, Kilimanjaro ilicheza mchezo mmoja wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Burundi na kufanikiwa kupata ushindi wa magoli 3-0.
Wanadada hao wa Tanzania bara waliwasili Uganda wakiwa tayari kukipiga kwenye michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa wanawake katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Tanzania iliangukia kwenye Kundi B kundi lililokuwa na timu tatu (Tanzania, Rwanda na Ethiopia).
Ilianza kwa ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Rwanda kisha ikatoka suluhu na Ethiopia na kufanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali kwa matokeo ya kurushwa shilingi kufuatia kulingana pointi na Ethiopia.
Kwenye husu fainali wakakutana na wenyeji wa mashindano hayo timu ya Uganga ambapo Kilimanjaro ikafuzu hatua ya fainali kwa kuichapa Uganda kabla ya kuishindaKenyanakutangazwa mabingwa wa CECAFA ya wanawake.

 CHANZO SHAFFIH DAUDA

MINO RAIOLA ARUSHA KIJEMBE KWA ARSENAL JUU YA POGBA

Wakala wa Paul Pogba Mino Raiola amezungumzia uhamisho wa mchezaji wake kwenda Manchester United, na kudai kwamba ingekuwa rahisi pia kwenda Real Madrid, lakini akiondoa uwezekano wowote wa mchezaji huyo kwenda Arsenal kwa kusema timu hiyo haina soka la kuweza kuvutia usajili wa mchezaji wa kiwango cha dunia.
Raiola amesisitiza kwamba ni kweli Arsenal wana pesa za kufanya usajili huo na kuonesha heshima yake waziwazi kwa Arsene Wenger, japokuwa anaamini timu hiyo imekosa kujiamini pale linapokuja suala la usajili wa wachezaji.
“Hapa sizungumzii tu suala la matumizi ya pesa,” Raiola ameliambia gazeti la Daily Mail. “Ni suala la kufanya maamuzi na kusema ‘ndio huyu ni mchezaji wangu’. Arsenal wana pesa, lakini wana mpira wa kuvutia wachezaji?
“Namheshimu sana Arsene Wenger. Ana falsafa ambazo anapenda kuzitumia ambapo hupenda kusema kiasi ninacholipa hakiendani na thamani ya mchezaji, lakini sio mbaya hakuna shida. Najua vizuri kwamba Wenger anampenda Pogba lakini bei ambayo Juventus waliiweka kumuuza mchezaji huyo haiendani na falsafa zake.
“Kwa upande wa Real Madrid, Zidane alikuwa tayari kwa kila kitu lakini hatukuwa na uhakika kama klabu yake ilikuwa ina mtazamo kama wake. Manchester United walitutumia message na kusema: ‘hii ni klabu kubwa duniani, hakuna tunachoweza kushindwa’.

”CHANZO SHAFFI DAUDA

SERENGETI BOYS IMEWATENDEA HAKI WATANZANIA – NNAUYE

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye amesema Serengeti Boys imewatendea haki watanzania kwa kushinda mechi yao ya nyumbani dhidi ya Congo Brazzaville.
“Vijana wamewatendea haki watanzania, tulijaa uwanjani kuwashangilia wamefanya kazi nzuri sana. Timu waliyopambana nayo ni timu nzuri lakini kwa matokeo waliyoyapata ni kutokana na kazi nzuri, mimi nawashukuru nawaombea heri kwenye mchezo unaofuata tunaamini watafanya vizuri”, alisema Mh. Nnauye mara baada ya mechi kumalizika na Serengeti kuibuka na ushindi wa magoli 3-2.
Serengeti inatarajia kucheza mechi yake ya marudiano dhidi ya Brazzaville baada ya wiki mbili huku ikiwa na matumaini ya kukata tiketi ya kusonga mbele kwenye mashindano hayo baada ya kushinda mchezo wa kawanza.CHANZO SHAFFII DAUDA

Amis Tambwe anasimama pekee na magoli yake 58 VPL

MSHAMBULIZI wa klabu ya Yanga SC, Mrundi, Amis Tambwe alifunga goli lake la tatu msimu katika ushindi wa Mwadui FC 0-2 Yanga.
Tambwe ameshatwaa mara mbili tuzo ya ufungaji bora wa ligi kuu Tanzania Bara katika misimu mitatu iliyopita alianza kufungua akaunti yake ya magoli wiki iliyopita alipofunga mara mbili katika ushindi wa Yanga 3-0 Majimaji FC hadi sasa amefikisha jumla ya magoli 58 katika ligi kuu pekee.
Alifunga jumla ya magoli 19 katika msimu wake wa kwanza ambao alishinda tuzo ya ufungaji bora akiwa na kikosi cha Simba SC msimu wa 2013/14.
Msimu wake wa pili alianza kwa kufunga katika sare ya Simba 2-2 Coastal Union mwezi Septemba 2014, lakini hadi anajiunga na Yanga kama mchezaji huru mwishoni mwa mwezi Desemba 2014 mshambulizi huyo hakuwa amefunga goli lolote.
Mambo yalianza kumnyookea tena kwani alifanikiwa kufunga jumla ya magoli 14 akiwa Yanga na kufikisha magoli 15 kufikia mwisho wa msimu wa 2014/15.
Msimu wake wa pili alimaliza katika nafasi ya pili ya ufungaji nyuma ya mchezaji mwenzake wa Yanga, Saimon Msuva ambaye alishinda tuzo hiyo baada ya kufunga magoli 17. Msimu uliopita (2015/16,) Tambwe alishinda kwa mara ya pili tuzo ya ufungaji bora baada ya kufunga jumla ya magoli 21.
Mrundi huyo ni hatari kwa mipira ya kichwa na amekuwa na shabaha ‘isiyokwisha’ anapopiga shuti golini. Baada ya kusainiwa kwa Mzambia, Obrey Chirwa ilidhaniwa labda utakuwa mwisho wa kutamba kwa Tambwe lakini tayari ameonesha bado ana njaa ile ile tu.
Huyu ni mshambuliaji-mfungaji bora zaidi katika ligi ya Tanzania Bara katika kipindi cha miaka 16 iliyopita. Ni mfungaji ambaye si rahisi kupatikana, ana mwendelezo bora katika ufungaji msimu hadi msimu. Amis Tambwe anasimama pekee na magoli yake 58 VPL CHANZO SHAFII DAUDA

Tuesday, August 23, 2016

NANI BINGWA AJTC KATI YA DIPLOMA NA CERTIFICATE MECHI YA KIRAFIKI IJUMAA WIKI HII


Kikosi cha diploma kimejipanga vyema kuelekea mechi ya kirafiki dhidi ya certificate mechi itakayopingwa katika uwanja wa  fid force jijini arusha kunako siku ya ijumaa wiki

kuelekea mchezo huo mshambuliaji wa timu hiyo ya diploma rogers fedinard amesema kuwa wanaendelea kujifua vyema na mazoezi ili kuhakikisha wanaibuka mabingwa  na kujinyakulia kitita cha zawaadi

Katika mechi iliyopita diploma waliweza kuibuka na ushidi wa mabao 5-4 katika uwanja wa fid force jijini arusha na hivyo wanatamba na kusema wanakila sababu ya kuibuka na ushidi katika mechi hiyo

Kwa upande wake msemaji wa timu hiyo Erick felinyo amesema kikosi kipo imara na wamejipanga vyema na watahakikisha wanaibuka mabingwa na kwa upande wa majeruhi hakuna mchezaji aliye majeruhi

kikosi cha ajtc diploma kitakachovaana na certificate ni kipa atakuwa felix faustine ,richard ngailla. jastine mkata. salum juma langa .hababi mohamendi .erick wanjala. jaksoni mabula . deogratusi festo . na rogers fedinards